• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZIARA ya Mbunge wa jimbo la Tunduru kusini Mhe. Idd D. Mpakate kuona maandalizi ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari katika Kata ya Mbati.

Imewekwa : July 14th, 2024

Mbunge wa jimbo la Tunduru Kusini Mhe. Idd D. Mpakate, Diwani wa Mbati Mhe. Tayson, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Ndg. Chiza C. Marando aliambatana na timu ya wataalamu kutoka idara ya ujenzi, elimu sekondari na Mipango kwenda kukagua na kujiridhisha eneo lililotengwa pamoja na nguvu za wananchi zilizoanza kufanya shughuli za ujenzi wa shule tarajali katika kata ya Mbati

Ziara hiyo ya Jumamosi tarehe 13.7.2024 Mhe. Mpakate alitumia nafasi hiyo kuwaelezea wananchi namna serikali inayoongozwa na Daktari Samia Suluhu Hassani inavyowathamini wananchi wa Mbati na awamu hii imewapatia fedha kiasi cha shilingi 560,552,827 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari katika kata ya Mbati kitu ambacho wamekuwa wakiomba kwa muda mrefu.

Pichani ni Wananchi wa Kata ya Mbati wakiwa katika mkutano.

Diwani wa kata ya Mbati Mhe. Taisoni pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbati walimshukuru Mhe. Rais kwa kuwaletea fedha hizo, Mhe Mbunge kwa mapambano yake kuhakikisha anapata gawio kwa ajili ya wananchi wa Mbati. Walisisitiza kuwa hakuna shaka mradi huo utatekelezwa kwa wakati kadri ya maelekezo ya serikali.

Pichani ni Diwani wa kata ya Mbati Mhe. Taisoni

Aidha, Ndg. Marando alieleza kuwa atahakikisha kuwa anasimamia mradi huo usiku na mchana huku akisisitiza juu ya uwajibikaji wa kila mwananchi, kulinda na kutunza mali na vifaa vya ujenzi muda wote na hatofumbia macho wizi, upotefu au ubadhilifu wa aina yeyote ili ukamilike kwa wakati na ifikapo January 2025 wanafunzi waanze kusoma.

Kwa upande wake Mhandisi wa Halmashauri Eng. Ramadhani Magaila alitoa ufafanuzi wa namna jengo litavyokuwa kama maelekezo ya serikali yanavyosema, pia aliwaomba wananchi kushiriki vizuri hasa kwenye maeneo yanayohitaji nguvu za wananchi (20%) kama shughuli za kusafisha eneo, kuchimba msingi, kifusi pamoja na maji.

Kaimu Afisa Elimu Sekondari Mwl. Mussa Chandu aliwaomba wana Mbati kupokea kwa mikono miwili mradi huo kwa kuhakikisha wanaungana kuukamilisha kwa wakati na ifikapo January watoto waanze masomo huku akiwasisitiza umuhimu wa kuwapeleka watoto shule na kuwasimamia wamalize tofauti na hapo awali ambapo shule ilikuwa mbali.

Wananchi wa kata ya Mbati walimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha anawatengenezea miundombinu ambayo itarahisisha upatikanaji wa huduma ya Elimu kwa watoto wao.

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.