• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZAIDI ya Bilioni 6 kujenga Mradi wa Umwagiliaji Tunduru.

Imewekwa : July 15th, 2024

Katika hatua kubwa ya kuimarisha sekta ya kilimo na kuongeza uzalishaji wa chakula, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeidhinisha kuanza kwa mradi mkubwa wa umwagiliaji katika Kijiji cha Nambarapi, Kata ya Masonya, Wilaya ya Tunduru. Mkandarasi aliyepewa dhamana ya kutekeleza mradi huu ataanza kazi tarehe 29.07.2024, na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 18, kufikia tarehe 31 Desemba, 2025.

Makabidhiano ya mradi huu wenye thamani ya shilingi bilioni 6,314,477,066.00 baina ya Tume ya Taifa ya umwagiliaji kwa mkandarasi yamefanyika kwa sherehe za hadhara katika kijiji cha Nambarapi, zimehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Chacha, ambaye alikuwa akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed.

Pichani ni Mkandarasi akionyesha Hati aliyokabidhiwa

Katika hotuba yake Mhe. Chacha alisisitiza umuhimu wa mradi huu katika kukuza uchumi wa wilaya na kuboresha maisha ya wananchi. Na pia, alimsisitiza Mkandarasi aliyekabidhiwa mradi huu kutekeleza kwa muda uliopangwa huku akizingatia ubora waliokubaliana na serikali wakati wa kupokea mkataba wa kazi.

“Mradi huu ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuwekeza katika sekta ya kilimo na kuboresha maisha ya wananchi, ni mradi ambao ukikamilika vyema hautakuwa na msimu, utafanya kazi kwa kipindi chote cha mwaka” alisema Mhe. Chacha “kuimarika kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja ndio kuimarisha uchumi wa taifa zima”.

Aidha, akielezea Mradi huu Msaidizi wa Mradi-Skimu ya Nambarapi, Mhandisi Lusia Chaula alisema, kazi zitakazofanywa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa banio na tuta, ujenzi wa mfereji mkuu, ujenzi wa mfereji wa upili, ujenzi wa mfereji wa matupio, ujenzi wa barabara za mashambani, ujenzi wa vivusha maji, na ujenzi wa ofisi ya mhandisi.

Akizungumza katika Mkutano huo Diwani wa Kata ya Masonya Mhe. Bwanali ameahidi atahakikisha kata yake inatoa ushirikiano mkubwa huku akisisitiza mkandarasi kuwapa kipaumbele wananchi wa kata hiyo katika kazi ambazo zitajitokeza ambazo wataona zinawafaa wanakijiji.

Pichani ni Diwani wa Kata ya Masonya Mhe. Bwanali

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.