• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WATATU wafutwa uwanachama , Mndichana AMCOS

Imewekwa : March 12th, 2024

Chama cha Ushirika cha Msingi Mndichana (Mndichana AMCOS) kimewafuta uwanachama, wanachama watatu kutokana na utovu wa nidhamu na kutotimiza masharti ya chama, ikiwemo kutokuuzia mazao yao kwenye chama hicho.

Tukio hili lilitokea katika Mkutano Mkuu wa kawaida wa chama uliofanyika katika Kijiji cha Msinji, Kata ya Ligoma, lengo likiwa kujadili taarifa za chama kwa msimu wa 2023/2024.

Meneja Mkuu wa chama hicho, Bw. Hassani Bakari Makina, aliwasilisha changamoto zilizokikabili chama wakati wa msimu wa ukusanyaji korosho. Alisema wanachama watatu walishinikiza wakulima na wanachama wengine kutokuuzia mazao yao kwenye chama hicho na pia walihamasisha vurugu.

Bw. Makina alieleza kuwa kutokana na kutotimiza masharti ya chama na utovu wa nidhamu, bodi ya chama ilipendekeza kuwafukuza wanachama hao.

Afisa Ushirika, Ndg. Raymond Raphael, alifafanua kuwa kulingana na kanuni na masharti ya chama cha Mndichana, hatua zitachukuliwa dhidi ya watu wanaohusika na makosa hayo.

“Bodi imeleta mapendekezo kwenu wanachama, ninyi kama wamiliki wa chama mnatakiwa kufanya maamuzi kulingana na kanuni na Masharti ya chama chetu kama katiba inayotuongoza katika kusimamia chama chetu”

Wananchama walipiga kura kuamua kuhusu pendekezo la bodi, na kura nyingi zilionyesha wanachama hao wafutwe uwanachama.

Afisa Ushirika wa Wilaya ya Tunduru, Ndg. George N. Bisani, aliagiza bodi ya chama kuwaandikia barua wanachama hao wakielezwa makosa yaliyosababisha kufukuzwa kwao na kuwapa stahiki zao, kama vile hisa zao, ndani ya siku 90 tangu kufutwa kwa uwanachama wao.

Mkutano huo ulienda sambamba na Uchaguzi wa Bodi ya Chama hicho kama ilivyo taratibu ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika ya   kufanyika kwa uchaguzi kwa vyama vyote vya Ushirika Nchini Tanzania.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.