• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUSIMAMAIA DHIDI YA UNYANYASAJI WA KIJINSIA WILAYANI TUNDURU

Imewekwa : April 6th, 2024

Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Dini Wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuzuia unyanyasaji wa kijinsia katika Mazingira yanayowazunguka.

Wito huu umetolewa katika semina iliyofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, ambapo viongozi hao walikutana kujadili ustawi wa jamii kupitia mshikamano wa madhehebu ya dini.

Mada kuu iliyowasilishwa katika semina hiyo ilihusu "Namna Bora ya Kuzuia Unyanyasaji wa Kijinsia katika Mazingira Yanayomzunguka Mwanadamu."

Akizungumza wakati wa semina hiyo, Meneja wa Mradi wa Kuimarisha Mshikamano Miongoni mwa Madhehebu Mbalimbali ya Dini, Ndg. Erick Gallawa, alisisitiza jukumu la viongozi wa dini katika kuzuia unyanyasaji wa kijinsia kutokana na nafasi yao kubwa ya kuaminika katika jamii.

Naye, Mwenyekiti wa mradi huo, Erasto Kitie, aliwapongeza viongozi wa dini kwa mawasilisho mazuri na kuwaomba kuendelea kutoa elimu kwa jamii kupitia njia mbalimbali kama vile mashuleni, nyumba za ibada, na ofisi za serikali ili kujenga jamii bora.

Kwa upande wake, Mchungaji Torben Madsen, Katibu Mkuu wa International Aid Services kutoka Denmark, alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, na kusisitiza umuhimu wa viongozi wa dini kusimama pamoja katika shughuli zao za kijamii ili kuendeleza amani na mshikamano katika jamii.

Mafunzo hayo yalifungwa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Ndg. Fadhili Chidyaonga, ambaye ni Mratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, ambaye alishukuru mradi huo kufika katika halmashauri ya Tunduru na kuelezea faida zilizopatikana kwa viongozi wa madhehebu ya dini katika kujifunza namna ya kushirikiana katika mambo mbalimbali.

Kwa upande wa viongozi wa madhehebu ya dini walioshiriki semina hiyo, Stephen Makina alisisitiza jukumu lao la kushirikiana na serikali katika kukemea unyanyasaji wa kijinsia kwa kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.