• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UZIO wa Pilipili Kupunguza Migongano ya Wanyamapori na Binadamu Tunduru.

Imewekwa : July 3rd, 2024

Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kupitia Serikali ya Ujerumani (BMZ) limeanzisha mradi katika Wilaya ya Tunduru unaolenga kupunguza migongano ya binadamu na wanyamapori, hasa uvamizi wa tembo katika mashamba ya wakazi.

Kabla ya mradi huu, wakazi walikuwa wakipambana kulinda mazao yao kwa njia za jadi, kama vile kupiga kelele na kutupa mawe ili kuwafukuza tembo wanapoingia mashambani, lakini mara nyingi njia hizi hazikuwa na ufanisi. Hii ilisababisha hasara kubwa kwa mazao na hata kusababisha majeraha na vifo kwa baadhi ya watu.

Mmoja wa Askari wa Uhifadhi wa Kijiji (VGS), Bw. Yassin Mkwanda, anaelezea mafanikio ya mradi huo: "Tunashukuru GIZ kwa kutusaidia kujenga uzio wa pilipili kulinda mashamba yetu. Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi, tuna uwezo wa kukabiliana na wanyamapori hawa. Tunajaza chupa za maji na unga wa pilipili, ambao tembo wanachukia sana harufu yake, na kuziweka kwenye uzio wetu kwa kutumia kamba za mkonge."

Pichani ni Askari wa Uhifadhi wa Kijiji (VGS), Bw. Yassin Mkwanda

Hivi karibuni, vijana watatu kutoka kijiji cha Mbati wamehitimu mafunzo kutoka Kituo cha Mafunzo ya Uhifadhi wa Msingi ya Jamii (CBCTC) - Likuyu Sekamaganga kilichopo Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma. Vijana hawa wameanza kutumia maarifa waliyopata kuwafundisha wakazi wengine njia za kuwafukuza tembo wanapoingia mashambani. Hii itasaidia kuhakikisha uendelevu wa kuimarisha uwezo wa jamii kukabiliana na changamoto za wanyamapori.

Pichani ni Askari wa Uhifadhi wa Kijiji (VGS)

Afisa Wanyamapori na Maliasili wa Wilaya ya Tunduru, Bw. Dunia Almas, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kupunguza migongano kati ya wanyamapori na binadamu. Amesema uzio wa pilipili umepunguza changamoto hii kwa asilimia 85.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Bw. Bosco Mwingira, anasema matukio ya uvamizi wa mashamba yanaongezeka hasa wakati mazao yanapokuwa yanakomaa, na kuvutia wanyama hao. Anaongeza kuwa Wilaya inatenga shilingi milioni 15 kila mwaka kununua vifaa vya kuwatisha na kuwafukuza tembo. Bw. Mwingira pia anataja kuwa ukusanyaji wa mapato ya wilaya umeongezeka kutoka shilingi bilioni 4.8 hadi bilioni 5.6, ambapo sehemu kubwa ya fedha hizo hutumika kutoa huduma za kijamii.

Pichani ni Bw. Bosco Mwingira ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.