• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TUNDURU yaendelea kuonesha nia ya kutatua migongano kati ya wanyamapori na binadamu.

Imewekwa : July 17th, 2024

Katika juhudi za kudumu za kulinda wananchi na mali zao dhidi ya migongano na wanyamapori, hasa tembo, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imeendelea kutoa mafunzo ya vitendo kwa wananchi wa vijiji vya Matemanga na Changarawe. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea uwezo wa kutumia uzio wa pilipili na vilipuzi kama njia bora za kuzuia migongano.

Mafunzo haya yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali ngazi ya Tarafa, Kata, kijiji pamoja na Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Matemanga, wote waliahidi kutoa ushirikiano wa kina ili mafunzo haya yaweze kuleta tija katika jamii na yafanikiwe ili kuepuka migongano baina ya binadamu na wanyamapori.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Bwana Dunia Almas, ambaye ni Kaimu Afisa Maliasili na Hifadhi ya mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, amewataka wananchi kuzingatia kwa makini mafunzo haya ili waweze kuyatumia katika maisha yao ya kila siku. Amesisitiza umuhimu wa kutenga maeneo maalumu ya kilimo ili kuepuka kuingia katika hifadhi za wanyamapori. Aidha, Bwana Almas amewakumbusha wananchi juu ya umuhimu wa kulima zao la pilipili, ambalo limeonekana kuwa na ufanisi katika kuzuia wanyamapori kuingia katika mashamba.

Mafunzo haya yaliandaliwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Hifadhi ya Taifa (TANAPA) na Pams Foundation. Ushirikiano huu unaonyesha dhamira ya pamoja ya kulinda mazingira na kuhakikisha kuwa wananchi wanaishi kwa amani na wanyamapori.

Mpaka sasa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ikishirikiana na wadau mbalimbali imefanya mafunzo katika vijiji 12, ambapo pamoja na mafunzo hayo pia imeweza kugawa vifaa ambavyo vitasaidia wananchi katika kupunguza migongano hiyo.

Serikali inaendelea kutoa wito kwa wananchi wote kuunga mkono juhudi hizi za kulinda mazingira na kuishi kwa amani na wanyamapori. Kupitia mafunzo haya, inatarajiwa kuwa idadi ya migongano itashuka na wananchi wataweza kuendelea na shughuli zao za kila siku bila wasiwasi.

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.