• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TUME kulinda Rasilimali ya Ardhi Tunduru.

Imewekwa : September 5th, 2023

TUME ya Taifa ya Mpango wa matumizi bora ya ardhi (National Land Use Planning Commisio-NLUPC) imeendesha zoezi la kupendekeza, kutathmini na upimaji wa ardhi kwa matumizi mbalimbali katika Wilaya ya Tunduru.

Mpango huu wa Tume umepitia katika vijiji nane katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ambavyo ni kijiji cha Muhuwesi, Liwangula, Ngapa,Chawisi, Mnazi mmoja,Matemanga,Ligunga na Jaribuni.

Lengo la zoezi hilo ni kuboresha matumizi ya ardhi nchini kwa kuweka mpango madhubuti unaolinda na kusimamia rasilimali ardhi kwa ajili ya matumizi endelevu. Zoezi hili litasaidia kukabiliana na migogoro ya ardhi baina ya watumiaji mbalimbali, vile vile kuwezesha upatikanaji wa Ardhi kwaajili ya uwekezaji katika maeneo hayo.

Akizungumza Bi Pili Msati ,Msimamizi wa kanda nyanda za juu Kusini -(NLUPC), alieleza kuwa , lengo la Serikali ni kujenga uelewa kwa wananchi wa maeneo ambayo yana muingiliano wa matumizi ya ardhi ,ili kuweka matumizi bora na sahihi ya ardhi kwa watumiaji tofauti.

"Tume imekuja kuwezesha mipango kwa lengo la kuweka sawa wastani wa matumizi ya ardhi,lazima tuhakikishe kwamba wananchi wanaishi kwa kuheshimu hifadhi na sehemu zote za ardhi zilizotengwa kwa matumizi maalumu”. Alisema.

Aidha Mpima Ardhi (W) Tunduru Ndg. Jeremia Nhambu, ameishukuru Serikali kwa kuleta mpango huu, kwani litasaidia kukabiliana na migogoro ya matumizi ya ardhi baina ya watumiaji mbalimbali hasa ya wafugaji na wakulima kwa njia ya Amani na haki. Pia, ameongezea kwa kuwakaribisha wawekezaji kwani mpango huu unaainisha maeneo ya uwekezaji katika maeneo yaliyoainishwa.

Pia kwa upande wao wananchi wa vijiji vilivyopitiwa na mpango huo ,wameishukuru Serikali kwa mpango huo kwani utapunguza migongano  kati ya wakulima na wafugaji, pia wamehaidi kulinda na kufuata mpango huo wa  Matumizi Bora ya Ardhi.

Mpango mzuri wa matumizi ya ardhi unaweza kuvutia wawekezaji kwa kutoa mwongozo wa maendeleo ya muda mrefu. Hii inawahakikishia wawekezaji kuwa siasa ya ardhi za eneo hilo ni thabiti na ina misingi ya kisheria, ambayo inaongeza Imani yao katika uwekezaji.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.