• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Tasaf Kubadilisha Uchumi wa Walengwa

Imewekwa : April 2nd, 2018

TASAF III ni muendelezo wa awamu mbili za mrdi wa kunusuru kaya maskini  Nchini, mpango huu unalenga katika kumuwezesha mwananchi mwenye hali duni ya maisha kuweza kujikwamua, kupata ahueni katika masuala ya lishe, afya na elimu.

Halmashauri ya wilaya ya tunduru ni miongoni mwa halmashauri nyingi nchini mambazo zinatekeleza mradi wa kunusuru kaya maskani na katika awamu ya tatu ambayo imeanza mwaka 2014 jumla ya kaya 15,813 zilibainishwa na kuanza kunufaika na ruzuku ya afya,elimu na lishe.

Taarifa inaendelea kutanabaisha kuwa walengwa wanashiriki katika shughuli mbalimbali za kuwaletea maendeleo walengwa ili kuweza kuondokana kabisa na umasikini, ikiwa ukarabari wa miundombinu, ujenzi wa vituo vya kutoa huduma za afya, na kazi nyingine kama ufugaji, kilimo na biashara ndogondogo.

Katika ajira za muda mfupi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya wilaya ya Tunduru imefanya kazi kazi mbali mbali ikiwa ni pamoja na upandaji wa miti ya matunda,mbao na ile ya kutunza vyanzo vya maji kuzunguka vyanzo vya maji.

Kisima cha maji katika kijiji cha lijombo kikiwa katika hatua za ukarabati, kazi iliyofanywa kwa ushirikiano wa Idara ya maji na Idara ya maendeleo ya Jamii inayosimamia utekelezaji wa mradi kunusuru kaya maskini.

sambamba na hayo walengwa walishiriki katika ukarabati wa visima vya maji ili kurahisha upatikanaji wa maji na kawawezesha walengwa kuweza kushiriki katika shughuli za kiuchumi. "katika kile kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 tumefanikiwa kukarabati isima cha maji katika kijiji cha lijombo, utengenezaji wa lambo la kuhifadhia maji ya mvua ili kipindi cha kiangazi kurahisisha wananchi kupata maji, kusimamia uchimbwaji wa mabwawa ya kufugia samaki" alisema mrtibu wa Tasaf wilaya Ndg Muhidin Shaibu.

wanufaika wa kaya maskini wilayani Tunduru wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kazi za ajira za muda zinazotolewa na Tasaf ili kuwaongezea walengwa kipato.

Utokomezaji wa hali duni kwa wananchi wa wilaya ya Tunduru unawezekana kwa viongozi kushirikiana na wananchi kwa karibu na kutoa elimu ya namna bora ya kilimo bora cha kisasa, ufugaji wa kisasa na wenye tija, hivyo wataalamu wa kilimo, mifugo na ustawi wa jamii wahamasishe wananchi kuona umuhimu wa kushiriki katika uzalishaji mali zaidi ya kuwa na mawazo kuwa serikali inafanya kila jambo


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.