• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TAMCU LTD yafanya Mkutano wa 21

Imewekwa : May 19th, 2024

Chama Kikuu cha Ushirika wa Masoko ya Mazao Tunduru (TAMCU LTD) kimefanya Mkutano Mkuu wa 21,Mei 18, 2024, katika Wilaya ya Tunduru.

Mkutano huo ulifanyika mjini Tunduru na ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa vyama vya ushirika, na wanachama wa TAMCU kutoka vyama vya Ushirika vya Msingi vyote vilivyopo wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Simon K. Chacha, alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo. Katika hotuba yake, Mhe. Chacha aliwataka viongozi wapya wa TAMCU kusimamia kwa ufanisi mambo na mikakati waliyoahidi kwa wanachama wao.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya viongozi na wanachama, na akawataka wanachama kuchagua viongozi waadilifu watakaowezesha ushirika kufikia maendeleo endelevu.

ā€œMaendeleo ya Ushirika yanahitaji ushirikiano,uadilifu na uaminifu, hivi vyote vinatakiwa kuanza kutengenezwa na sisi viongozi wenyewe.Alisema Mhe,Chacha.

Mkutano huo ulienda sambamba na Uchaguzi wa kupata bodi mpya ya uomgozi wa chama kikuu cha ushirika Tunduru (TAMCU LTD).

Ambapo katika uchaguzi uliofanyika, Ndg. Mussa Athumani Manjaule alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi mpya ya TAMCU, Bodi ambayo inaundwa na wajumbe sita.

Katika hotuba yake baada ya kuchaguliwa, Ndg. Manjaule aliwashukuru wanachama kwa kumwamini tena kuwa kiongozi wao. Aliahidi kutekeleza mikakati yote ya TAMCU kwa lengo la kuimarisha ushirika na kuleta maendeleo kwa wanachama wake. Pia aliahidi kushirikiana kwa karibu na watumishi wa TAMCU ili kuhakikisha maendeleo endelevu ya chama hicho.

Mkutano huo pia uliishuhudia uzinduzi wa magari mawili mapya ya mizigo aina ya Scania yaliyonunuliwa na vyama vya ushirika vya msingi vya SAMA AMCOS na NGUVUMALI AMCOS kwa ushirikiano na benki ya CRDB. Magari hayo yananatarajiwa kurahisisha usafirishaji wa mazao ya wakulima kutoka vijijini hadi masoko, na hivyo kuboresha maisha yao.

Kwa ujumla, Mkutano Mkuu wa 21 wa TAMCU ulikuwa wa mafanikio makubwa. Uchaguzi wa bodi mpya unatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika ushirika huo, na uzinduzi wa magari mapya ya mizigo utasaidia kuboresha maisha ya wakulima katika Wilaya ya Tunduru.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.