• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

NAIBU Katibu Mkuu, Elimu (OR TAMISEMI) afanya mazungumzo na Walimu Tunduru.

Imewekwa : November 21st, 2023

Naibu Katibu Mkuu, Elimu (OR TAMISEMI) Dkt. Charles Msonde, amefanya mkutano na walimu wa wilaya ya Tunduru, mkoani Ruvuma. Mkutano huo ulihudhuriwa na walimu kutoka shule zote za msingi na sekondari za wilaya ya Tunduru.

Akizungumza katika mkutano wa walimu wa wilaya hiyo uliofanyika tarehe 21 Novemba 2023, Mwl. Nkwama alisema kuwa uadilifu ni nguzo muhimu katika utendaji kazi wa walimu, na kwamba walimu wanapaswa kuwa waadilifu katika kila jambo wanalofanya, ikiwa ni pamoja na kufundisha, kutathmini wanafunzi, na kusimamia taarifa za wanafunzi.

“Walimu wangu mnafanya kazi kubwa sana, tembeeni kifua mbele, msijipe presha katika utendaji kazi wenu, mnastahili pongezi za dhati” alisema Dkt. Msonde “Mwalimu ndio msingi wa fani na ujuzi wowote duniani, tunafanya kazi ya kulea watoto kwa kuzingatia misingi na maadili ya kitanzania, jukumu hili tuliachiwa na baba wa taifa, hayati Mwal. J.K. Nyerere”

Dkt. Msonde pia aliwasisitiza walimu wa wilaya ya Tunduru kujipanga kwa ajili ya mtaala mpya wa elimu utakaoanza kutumika kwa mwaka wa masomo 2024/2025. Alisema kuwa mtaala huo unalenga kuboresha ubora wa elimu nchini, na kwamba walimu wanapaswa kujifunza kuhusu mtaala huo ili waweze kuutekeleza kwa ufanisi.

Aidha, Dkt. Msonde alitoa ahadi ya kuhakikisha madeni yote ya walimu wa wilaya ya Tunduru yanalipwa, ikiwa ni pamoja na madeni ya uhamisho na likizo. Alitoa agizo kwa idara ya Elimu wilaya kuhakikisha kuwa madeni hayo yatalipwa haraka iwezekanavyo. Alisema kuwa Serikali inatambua mchango wa walimu katika maendeleo ya elimu nchini, hivyo inawajibika kuhakikisha kuwa wanalipwa stahiki zao kwa wakati.

Akihitimisha mazungumzo na walimu Dkt. Msonde, alilisisitiza juu ya wanafunzi wote waliohitimu darasa la saba kujiunga na masomo ya pre-form one ili waweze kupata maandalizi bora kabla ya kuanza masomo ya kidato cha kwanza. Ameongeza kuwa serikali ina nia ya kuhakikisha kuwa kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anapata elimu bora, hivyo ni muhimu kwa wazazi na walezi kuhakikisha kuwa wanawapeleka watoto wao shule.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.