• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MRADI wa stawisha maisha waja kukomesha udumavu Tunduru.

Imewekwa : July 10th, 2024

Mradi wa Stawisha Maisha unatarajiwa kuanzishwa hivi karibuni katika Wilaya ya Tunduru, ukiwa na lengo la kuwanufaisha akina mama wajawazito na wenye watoto chini ya miaka mitano (0-5). Mradi huu unalenga kuelimisha jamii kuhusu masuala ya lishe bora, hasa kwa watoto wadogo, katika mkoa wa Ruvuma unaojulikana kuwa na viwango vya juu vya udumavu licha ya kuwa na uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula.

Serikali kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto na wanawake katika mataifa yanayoendelea (UNICEF), imeweka mikakati ya kupambana na udumavu katika mkoa wa Ruvuma, Mradi wa Stawisha Maisha ni sehemu ya mikakati hii. Wilaya ya Tunduru ni miongoni mwa wilaya tatu zilizochaguliwa kushiriki katika mradi huu wa majaribio, wilaya nyingine ni pamoja na Wilaya ya Mbogwe-Geita, na Wilaya ya Kongwa iliyopo Mkoani Dodoma.

Akitolea ufafanuzi wa Mradi huu, Afisa ufuatiliaji wa Wilaya ya Tunduru kutoka makao makuu ya TASAF ambayo yapo Dar es salaam, Bw. Lazaro Mapimo alisema Mkoa wa Ruvuma, licha ya kuwa miongoni mwa mikoa inayozalisha mazao ya chakula kwa wingi, lakini una kiwango kikubwa cha hali ya udumavu. Hii inamaanisha kuwa watoto wengi hawapati virutubisho stahiki na vya kutosha kwa ukuaji na maendeleo bora.

“Mradi wa Stawisha Maisha unatarajiwa kuleta mabadiliko chanya kwa afya na ustawi wa mama na watoto katika Wilaya ya Tunduru. Kupitia elimu bora ya lishe, tunatarajia kupunguza viwango vya hali ya udumavu na kuboresha maisha ya jamii kwa ujumla” Alisema Bwn. Mapimo.

Mradi huu unapitia hatua za awali za kuunda vikundi vya walengwa. Pamoja na mafunzo mbalimbali watayopatiwa, wanachama wa vikundi hivi watapokea redio bure watakazotumia kusikiliza vipindi mbalimbali vya kuelimisha kuhusu lishe bora kwa mama na watoto.

Wananchi wa Wilaya ya Tunduru wanapewa wito kushirikiiana katika mradi huu kwa kuhamasisha akina mama wajawazito na wenye watoto chini ya miaka mitano kushiriki kikamilifu katika vikundi vitakavyoundwa na kusikiliza vipindi vya elimu ya lishe. Pamoja, tunaweza kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata lishe bora kwa ukuaji na maendeleo yao bora.

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.