• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MKUU wa Wilaya aongoza Mdahalo katika kuadhimisha Miaka 62 Uhuru Tanzania Bara.

Imewekwa : December 9th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Wakili, Julius S. Mtatiro ameongoza mdahalo wa kujadili mustakabali wa Wilaya ya Tunduru katika kilele cha maadhimisho ya miaka 62 ya uhuru wa Tanzania Bara.

Mdahalo huo ulihudhuriwa na viongozi wa vyama vya kisiasa, dini, wanafunzi, wazee maarufu na wakazi wa Wilaya ya Tunduru, ulilenga kuzungumzia mafanikio ambayo wilaya imeyapata kwa miaka 62 tangu Tanzania Bara kupata uhuru wake.

Pichani:Wanafunzi wakishiriki Mdahalo

Katika mdahalo huo washiriki walijadili masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Elimu, Afya, Kilimo, Maji na Miundombinu ya barabara. Pamoja na mafanikio yanayoendelea kupatikana kwa miaka 62 tangu Tanzania Bara ipate Uhuru wake, Wilaya ya Tunduru bado inahitaji kuwekeza Zaidi katika sekta ya kilimo ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya biashara na chakula. Vile vile, wilaya ya Tunduru inaendelea kujenga na kuboresha upatikanaji wa miundombinu ya Elimu na afya ili kuwaandaa wananchi kwa maendeleo na pia uwepo wa huduma bora za afya.

Akizungumza mara baada ya kuongoza mdahalo huo Mhe. Wakili, Mtatiro alisema kwamba maadhimisho ya Uhuru Tanzania Bara huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kukumbuka historia ya harakati za kudai uhuru wetu toka kwa wakoloni na mchango wa viongozi wetu. Hivyo, kuna kazi kubwa katika kuhakikisha tunalinda Uhuru, umoja na mshikamano kwakuwa pasipo na mshikamano ni vigumu sana nchi kupata maendeleo.

“Tumekuwa na watoa mada kutoka idara ya Elimu msingi na Sekondari, Afya, kilimo, RUWASA na TARURA, wametupitisha kule ambako tumetokea, tulipo na tunapoelekea katika maendeleo kama Wilaya kwa miaka 62 ya uhuru wa Tanzania bara” alisema “Nchi yetu imepiga hatua kubwa ukilinganisha wakati ule inapata uhuru mpaka sasa tunatimiza miaka 62, tumepata maendeleo makubwa sana na tija imeongezeka katika sekta mbalimbali”

Aidha, Baada ya Mdahalo huo kumalizika Mhe. Wakili, Mtatiro alieleza umuhimu wa uhuru wa Taifa la Tanzania, alisema taifa letu linaongozwa kwa kufuata misingi ya kidemokrasia na kuzingatia uhuru wa wananchi wake. Wananchi waliahidi kufanya kazi kwa pamoja ili kushirikiana na serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais wa awamu ya sita, Mhe. Daktari Samia Suluhu Hassan katika kuboresha maisha ya wananchi wa Wilaya ya Tunduru.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.