• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MHESHIMIWA,Mhandisi Kundo Aweka Jiwe la Msingi kwa Mradi wa Maji wa Bilioni 3 Tunduru.

Imewekwa : December 13th, 2024

Katika hatua kubwa ya kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa Wilaya ya Tunduru, Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, ameweka jiwe la msingi la mradi wa maji Msechela-Liwanga. Mradi huu utakaogusa maisha ya maelfu ya watu, unatarajiwa kukamilika kwa Zaidi ya Shilingi bilioni 3.02.

Akizungumza na Wananchi katika hafla hiyo, Mhandisi Kundo alisema kuwa mradi huu ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha kuwa wananchi wote wa Tanzania wanapata huduma bora ya maji safi na salama. Aliongeza kuwa mradi huu utanufaisha zaidi ya watu elfu tisa ambayo ni idadi kubwa ya wananchi wa maeneo hayo.

"Mradi huu ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuwekeza katika sekta ya maji. Tunatarajia kuwa baada ya kukamilika kwa mradi huu, wananchi wa eneo hili watakuwa na uhakika wa kupata maji safi na salama kwa matumizi ya kila siku," alisema Mhe.Mhandisi Kundo.

Kwa upande wao, wananchi wa Msechela-Liwanga wameipongeza Serikali kwa kuwajengea mradi huo ambao unatarajiwa kutatua changamoto ya uhaba wa maji ambayo wamekuwa nayo kwa muda mrefu. Wamesema kuwa mradi huu utawawezesha kupata muda mwingi wa kufanya shughuli nyingine za maendeleo badala ya kupoteza muda mwingi kutafuta maji.

Mradi huu unaotekelezwa na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) Ruvuma, unatarajiwa kumalizika mnamo tarehe 28.02.2025, na pia, unatarajiwa kurahisisha upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo haya, ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakikabiliwa na uhaba wa maji.

Pichani ni Meneja wa RUWASA Tunduru, Mhandisi, Maua Mgala akitoa ufafanuzi wa Mradi wa Maji wa Misechela-Liwanga

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.