• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Madiwani Tunduru Watakiwa Kutoa Ushirikiano Kwa Watendaji

Imewekwa : May 7th, 2019


Na: Theresia Mallya –Tunduru

Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma wametakiwa kutoa ushirikiano unaaostahili baina yao na watendaji wengine wa Halmashauri hiyo ili kuongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu yao.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Juma Zuberi Homera wakati akitoa salamu za Serikali katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Robo ya Tatu uliofanyika leo katika ukumbi wa klasta ya Mlingoti wilayani humo.

“Madiwani tukimuachia kila kitu Mkurugenzi na Mkuu wa wilaya ndio wasimamie na nyie kukaa pembeni hatutaweza kuwasaidia wananchi wetu kujikwamua na umaskini, nawaombeni Waheshimiwa Madiwani, tuungane pamoja na tuzungumze lugha moja katika kuiendeleza Tunduru kwani ni yetu sisi sote”, Alisema Juma Homera.

Homera amewataka Madiwani hao kufanya kazi kwa kushirikiana na Watumishi na Viongozi wengine wa wilaya hiyo ili kuongeza kasi ya ukuaji wa kiuchumi ili kufikia malengo ya uchumi wa Kati ifikapo 2025

Mkurugenz Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Gasper Z.Balyomi akitoa ufafanuzi wa hoja ya ukusanyaji mapato katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2019 uliofanyika leo katika ukumbi wa klasta Tunduru Mjini.

Alisema kuwa wakati wa kuunganisha nguvu ya pamoja katika usimamizi wa mapato ndani ya Halmashauri na kuhakikisha hakuna mfanyabiashara anakwepa kulipa kodi lakini pia kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha Mkuu wa Wilaya huyo aliongeza kuwa katika Msimu wa Kilimo wa Mwaka 2019 Serikali kupitia Bodi ya Mazao Mchanganyiko wakulima wa zao la Ufuta watanufaika kwa kuuza ufuta katika mfumo mpya wa stakabadhi ghalani kama walivyouza wakulima wa Mikoa ya Lindi na Mtwara Msimu wa Mwaka 2018.

Aliwajulisha madiwani Halmashauri kwa kushirikiana na Vyama vya Msingi watashirikiana katika usimamizi wa ununuzi wa zao utakaofanyika katika vyama vya msingi wilayani Tunduru.

Hata hivyo serikali kupitia bodi ya mazao mchanganyiko inajipanga kuona namna ya ununuzi wa mazao kama Karanga, Choroko,Mbaazi, Mpunga na Njugu kuwekewa mkakati wa kuingizwa katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili yalete tija kwa wananchi.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg. Gasper Zahoro Balyomi aliwataka Waheshimiwa Madiwani kutoka Kata zote kushiriki katika zoezi la usimamizi wa ununuzi wa mazao mbalimbali kwani Halmashauri imebainisha vituo vya kununulia mazao katika vijiji na kata zenu.

Mwisho.



Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.