• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KIKAO cha Lishe Ngazi ya Wilaya.

Imewekwa : July 30th, 2024

Kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa afua za lishe ngazi ya wilaya kimefanyika tarehe 30.07.2024 katika ukumbi wa klasta kata ya Mlingoti. Kikao hiki kiliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Chacha na kilihudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Tunduru Ndg. Chiza Marando, wakuu wa idara na vitengo, na watendaji wa kata.

Kikao kililenga kutathmini maendeleo yaliyofanywa katika utekelezaji wa mkataba wa afua za lishe, kubaini changamoto zinazoikabili sekta ya lishe, na kupanga mikakati ya kuboresha utoaji wa huduma za lishe katika wilaya.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Chacha aliwapongeza watendaji wa kata kwa juhudi kubwa walizoziweka katika kutekeleza mkataba wa afua za lishe. Alieleza kuwa amefurahishwa na mafanikio yaliyopatikana katika kupunguza udumavu katika baadhi ya kata.

“Endeleeni kuelimisha wananchi kujisimamia wenyewe hasa kwenye masuala ya Lishe bora, wasisubiri mpaka serikali ije ifanye” alisema “Wajitahidi kupambana kwa ajili ya afya zao wenyewe ili kuondoa hali ya udumavu”.

Mhe. Chacha alimpongeza Mtendaji wa kata ya Nakapanya Bi. Leocadia Mponda kwa ufanisi wake katika utendaji kazi wa maswala ya Lishe, pia, Bi. Leocadia alikabidhiwa cheti na kiasi cha shilingi 100,000 kama motisha ya kufanya kazi kwa bidii.

Pichani ni Mhe. Chacha akimkabidhi Cheti cha pongezi Bi. Leokadia Mponda.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya alibainisha kuwa bado kuna kazi kubwa ya kufanya. Aliwataka watendaji kuendelea kuimarisha ushirikiano ili kuweza kuondoa kabisa tatizo la udumavu katika wilaya. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuelimisha jamii kuhusu masuala ya lishe bora, kwani Mkoa wa Ruvuma unaojulikana kuwa na viwango vya juu vya udumavu licha ya kuwa na uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula.

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.