• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KAMATI ya siasa ya CCM Tunduru kukagua Miradi ya maji.

Imewekwa : November 28th, 2023

Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Tunduru ikiongozwa na Cde. Abdallah Mtila imetembelea majimbo ya Tunduru Kusini na Tunduru Kaskazini kukagua miradi ya maji mwezi Novemba, 27.

Miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Ndaje - Mbesa (Vijiji vya Mbesa, Lijombo na Airport), tarafa ya Nalasi, Mradi wa Misechela (Misechela na Liwanga), tarafa ya Namasakata, Mradi wa Maji kata ya Majimaji tarafa ya Nakapanya, Mradi wa Maji kata ya Masonya, tarafa ya Mlingoti, miradi hiyo ni miongoni mwa miradi mingi ya maji inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Kamati hiyo iliyoambatana na wajumbe wake ilitumia zaidi ya kilomita 389 kukagua na kujionea ufanisi wa miradi minne ya maji yenye thamani zaidi ya Shilingi Bilioni 4.8. Ukaguzi wa miradi hiyo ni katika utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambayo ni serikali ya awamu ya sita.

Aidha, Kamati imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Daktari, Samia Suluhu Hassan, Wizara ya Maji, RUWASA, viongozi wote na watendaji kwa juhudi kubwa za kuibadilisha wilaya ya Tunduru.

Miradi hiyo inatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Tunduru ndani ya miaka 5 ijayo,ambapo, kutokana na ukubwa wa miradi hii na mawanda yake, matatizo ya maji yatakuwa yamemalizwa kwa asilimia 90 kwenye wilaya kubwa.

Ukaguzi huu wa miradi unasaidia kutambua mapungufu yoyote katika utekelezaji wa miradi, na hatua za kurekebisha mapungufu hayo huchukuliwa mara moja. Ukaguzi huangalia utekelezaji wa miradi ya maendeleo hiyo kwa kuzingatia mambo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uwiano wa gharama na kazi iliyofanyika, ubora wa vifaa na kazi zilizofanywa, muda wa utekelezaji wa mradi na matumizi sahihi ya fedha za mradi.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.