• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma yatembelea miradi ya maendeleo Tunduru.

Imewekwa : October 4th, 2023

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo wilayani Tunduru, Miradi hiyo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD) lililopo katika Hospitali ya Wilaya, ujenzi wa Shule mpya, maabara, majengo ya Tehama, mabweni,na vyoo. Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa, Mhe. Komred Oddo Mwisho, na iliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Kanali, Labani Thomas.

Pichani (aliyeshika koleo): Mwenyekiti wa kamati ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa, Mhe. Komred Oddo Mwisho.

Baada ya kukagua miradi hiyo, Kamati iliridhika na utekelezaji wake. Komred Mwisho aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo, na pia aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa kusimamia vyema utekelezaji wa miradi hiyo. Alisema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umekuwa wa kuridhisha na unakwenda sambamba na maelekezo ya Serikali.

"Tumefurahishwa sana na utekelezaji wa miradi hii. Tunaipongeza Serikali kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo. Tunaamini kuwa miradi hii itasaidia kuboresha hali ya maisha ya wananchi wa Tunduru, Kwa kipindi kirefu watoto wetu wamekua wakipata shida kwasababu Shule zilikua mbali sana, lakini mpaka sasa karibia kila kata inapata shule” alisema Mhe. Mwisho. “Tunawapongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa kusimamia vyema utekelezaji wa miradi hii. Tunaamini kuwa ushirikiano huu utaendelea kuwepo ili kufanikisha miradi mingine ya maendeleo,"

Aidha, kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Kanali, Labani Thomas, aliipongeza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa kwa kufanya ukaguzi wa miradi hiyo. Na kuwa ukaguzi huo ni muhimu ili kuhakikisha kuwa miradi inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia viwango, aliahidi kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Ruvuma. Alisema Serikali ina dhamira ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii.

Pichani: Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Kanali Labani Thomas

"Ninaipongeza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa kwa kufanya ukaguzi wa miradi hii. Ukaguzi huu ni muhimu ili kuhakikisha kuwa miradi inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia viwango “. Alisema “Tutaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Ruvuma, ni wazi kwamba Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Daktari. Samia Suluhu Hassan, ina dhamira ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii,"

Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma katika wilaya ya Tunduru ni sehemu ya ziara inayoendelea katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.